Matola atumiwa nauli aingia mitini


MOJA ya makocha chipukizi wazawa ambao wanaaminika kuwa ni bora kwenye soka la Tanzania kwa sasa basi ni kocha msaidizi wa Simba Suleiman Matola ambaye amefanya mambo makubwa kadhaa kwenye soka la Tanzania.


Matola ambaye aliweka baadhi ya rekodi akiwa na Lipuli ya Iringa sehemu ambayo alitambulika sana, lakini pia akawa na Polisi Tanzania na kufanya tena mambo makubwa akiwa na Simba, siyo jina geni sana baada ya kukaa pia kwenye kikosi cha Simba kwa muda mrefu.



Amepitia mambo mengi akiwa na Simba, kuna wakati ameonja joto ya jiwe kutoka kwa mashabiki, kuna wakati ameshangiliwa na mashabiki haohao, hawa ndiyo watu wa soka, lakini katika maisha ya soka, Matola ana mambo mengi ambayo wengi hawayajui kwa kuwa siyo muongeaji sana na mara nyingi imekuwa ikielezwa kuwa ni mtu msiri sana kuhusu maisha yake ya nyuma ya soka.

ليست هناك تعليقات:

إرسال تعليق